HEART TO GOD HAND TO MAN

Friday, September 26, 2025

HOTUBA YA SHEREHE MIAKA 25 YA CHUO CHA MAFISA - TANZANIA TERRITORY {2000-2025}

 

                                          COLONEL SAMUEL MKAMI


        Bwana Yesu asifiwe wana wa Mungu, Maafisa, Makadeti, na wafanyakazi,  na ndugu zetu wote katika Kristo, 


Kwa furaha na shukrani kuu, tunasimama mbele ya Mungu leo hii kuadhimisha miaka 25 ya chuo chetu cha maafisa tangu chuo hiki kianzishwe mwaka 2000. Ni neema kubwa na si kwa uwezo wetu, bali ni kwa mkono wa Mungu aliyetuongoza hatua kwa hatua mpaka tumefika hapa. 


Kwanza, tunamshukuru Mungu Baba yetu kwa kuwa ndiye aliyepanda mbegu ya wito wa kuanzisha chuo  hiki. Kupitia maono ya waanzilishi na uongozi wa Kanisa, ulikuwa kuwa ni lazima kanisa liwe na viongozi waliofundishwa vizuri ili kubeba maono ya mwokozi wetu na kufanya ukristo uwe na thamani kubwa mioyoni mwa watu wa Mungu. Na waanzilishi wetu walianzisha huduma hii 

chuo hiki kimekuwa chombo cha baraka na huduma kwa teritori ya Tanzania. 


Pili, napenda kutoa shukrani za dhati kwa viongozi wa Kanisa hasa Lieut-Colonel David na Jean Burrows, Major Linda Manhardt pia Commisioner Patricia Bird kwa mpango mzuri wa kuanzisha chuo hiki. Na hasa General John Gowans aliyeidhinisha uanzishwaji wa chuo hiki.  Tunawashukuru maafisa walimu, wahitimu, na wadau wote walioweka nguvu, muda, na maombi kuhakikisha chuo hiki kinasimama imara kwa robo karne. Bila mshikamano huu wa kiimani, safari hii isingefanikishwa. 


Katika kipindi cha miaka 25, tumeona: 


Watakaji wliitika mwito kusoma Neno la Mungu na kujifunza huduma na uongozi wa kiroho. 


Wahitimu wengi wakitumwa kwenye vikao na matuo mbalimbali, wakiwa mashuhuda wa Kristo. Na kwa kupitia kwao kanisa limeendelea kukua na kuimarika. 


Lakini tunakumbuka pia kwamba mafanikio haya si kwa ajili ya kujivunia tu, bali ni wito wa kuendelea kuwa mwangaza wa mataifa na chumvi ya dunia. Tunaposherehekea miaka 25, tujiulize: je, tunazidi kusimama kwenye msingi wa Neno la Mungu? Je, tunazalisha wachungaji na viongozi wenye moyo wa Kristo aliye mchungaji mwema? 


Tunapoitazama safari ijayo, tunahimizwa na maneno ya Mtume Paulo kwa Wafilipi 3:13-14: “Sijasahau mambo yaliyo nyuma, lakini nakaza mwendo, nikikazia shabaha ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu.”

Hivyo, safari ya miaka 25 inayofuata iwe safari ya uaminifu zaidi, unyenyekevu, matumaini, maendeleo na kujitolea kwa huduma. 


Kwa Makadeti, na , kumbukeni ninyi ndio matunda ya chuo hiki. Msije kusahau kwamba elimu ya kichungaji si kwa ajili ya heshima, bali ni kwa ajili ya huduma. Mmeitwa si tu kujifunza, bali pia kuwa mifano ya maisha ya Kristo katika jamii zenu kuanzia sasa na siku zijazo. 


Mwisho, napenda kusema: Jubilei hii ya miaka 25 iwe kumbukumbu kwamba “Aliyeanza kazi njema ndani yetu ataikamilisha hata siku ya Kristo Yesu” (Wafilipi 1:6). Tumsifu Mungu kwa uaminifu wake wa jana, leo, na kesho. 


Tunapoanza sherehe hizi tujikumbushe maneno ya ushindi wa waisraeli na tendo kubwa lililofanyika huko Mispa wakati wa nabii Samweli. 


1 Samweli 7:12 


Andiko linasema: 


“Ndipo Samweli akatwaa jiwe, akalisimika kati ya Mispa na Sheni, akaliita jina lake Eben-ezeri, akisema, Hata sasa Bwana ametusaidia

COLONEL SAMUEL MKAMI
TERRITORIAL COMMANDER

25TH ANNIVERSARY CEREMONY OF THE OFFICERS' COLLEGE -{2000 - 2025} TANZANIA TERRITORY

                                       COLONEL SAMUEL MKAMI

May the Lord Jesus be praised by the children of God, Officers, Cadets, and staff, and all our brothers in Christ, 

With great joy and gratitude, we stand before God today to celebrate 25 years of our officers' college since its inception in 2000. It is a great blessing and not by our own ability, but by the hand of God who guided us step by step until we have arrived here. 

First, we thank God our Father for planting the seed of the call to establish this college. Through the vision of the founders and the leadership of the Church, it was imperative that the church have well-trained leaders to carry the vision of our savior and make Christianity a great value in the hearts of God's people. And our founders established this ministry 
this college has become an instrument of blessing and service to the territory of Tanzania. 

 Secondly, I would like to express my sincere gratitude to the leaders of the Church, especially Lieut-Colonel David and Jean Burrows, Major Linda Manhardt, and Commissioner Patricia Bird, for their excellent initiative in establishing this college. And especially to General John Gowans, who approved the establishment of this college. We thank the officers, teachers, graduates, and all stakeholders who have put in the energy, time, and prayers to ensure that this college has stood strong for a quarter of a century. Without this unity of faith, this journey would not have been possible. 

Over the past 25 years, we have seen: 

Aspirants respond to the call to study the Word of God and learn about ministry and spiritual leadership. 

Many graduates are sent to various forums and events, as witnesses for Christ. And through them, the church has continued to grow and strengthen. 

But we also remember that these achievements are not just for pride, but are a call to continue to be a light to the nations and the salt of the earth. As we celebrate 25 years, let us ask ourselves: are we increasingly standing on the foundation of the Word of God?  Are we producing pastors and leaders with the heart of Christ the Good Shepherd? 

As we look to the journey ahead, we are encouraged by the words of the Apostle Paul in Philippians 3:13-14: “I do not forget those things which are behind, but I press on toward the goal for the prize of the upward call of God in Christ Jesus.”
Thus, may the next 25-year journey be one of greater faithfulness, humility, hope, progress, and dedication to service. 

To the Cadets, and , remember that you are the fruit of this college. Lest you forget that pastoral education is not for honor, but for service. You are called not only to learn, but also to be examples of the life of Christ in your communities from now on and into the future. 

Finally, I would like to say: Let this 25-year jubilee be a reminder that “He who began a good work in you will complete it until the day of Christ Jesus” (Philippians 1:6). Let us praise God for His faithfulness yesterday, today, and tomorrow. 

 As we begin these celebrations, let us remember the words of the victory of the Israelites and the great deed that took place at Mizpah during the time of the prophet Samuel. 

1 Samuel 7:12 

The text says: 

“Then Samuel took a stone and set it up between Mizpah and Shen, and called its name Ebenezer, saying, ‘Thus far the Lord has helped us' 

 COLONEL SAMUEL MKAMI
TERRITORIAL COMMANDER

Wednesday, June 11, 2025

THE SALVATION ARMY MATUMAINI PRIMARY SCHOOL

MATUMAINI PRIMARY SCHOOL SALVATION ARMY MATUMAINI PRIMARY SCHOOL Matumaini is a primary boarding school for disabled and albino children. Operating for over 20 years, Matumaini is the largest school of its kind in the country. Nearly 200 children are attending the school from communities around the Tanzania. Located at the Salvation Army property in Temeke, Matuamaini maintains the highest educational standards as set by the Ministry of Education. But in addition to education, we provide physical therapy and we operate a workshop for the manufacturing and repair of walking appliances and chairs. Children are a gift from the Lord, and we are proud to be the guardians of these precious children, and our pray for all of them is that they would reach their potential as contributors to society in Tanzania For more information, please contact us +255742592621